Tuesday, August 7, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ATEMBELEA MABANDA YA MAONYESHO YA NANE NANE DODOMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo jinsi ya uzalishaji wa zao la Zabibu kutoka kwa Ofisa Mtafiti Msaidizi wa Kilimo wa Kanda ya Kati Dodoma, Richard Malle, (wa pili kulia) wakati Makamu alipotembelea katika Banda la Kilimo Kwanza, maonyesho ya Nane Nane kwenye Viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma jana Agosti 6, 2012. Wa kwanza (kushoto) ni Naibu Waziri wa Chakula na Ushirika, Adam Malima. Kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti wa Kilimo, Kanda ya Kati Dodoma, Leon Mroso. Picha na Muhidin Sufiani-OMR.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, mkewe Mama Zakhia Bilal, Naibu Waziri wa Chakula na Ushirika, Adam Malima, wakiangalia Mhogo aina ya Mumba wenye umri wa miaka (3) wakati Makamu alipotembelea katika Banda la Kilimo Kwanza, maonyesho ya Nane Nane kwenye Viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma jana Agosti 6, 2012.Wa pili (kulia) ni Mke wa Makamu, Mama Zakhia Bilal na wa kwanza (kushoto) ni Naibu Waziri wa Chakula na Ushirika, Adam Malima.Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo jinsi mashine za kukamulia miwa zinavyofanya kazi, kutoka kwa Mjasiliamali, Patrisia Kisabua, wakati Makamu alipotembelea katika Banda la Kiwanda cha Sukari, maonyesho ya Nane Nane kwenye Viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma jana Agosti 6, 2012.Kushoto ni Naibu Waziri wa Chakula na Ushirika, Adam Malima. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
 Batrez asema yanga ni kama baba na mama kwani kuja kwake yanga kutafungua ufungua wa maisha yake katika soka tafauti na alipokuwa zamani kwania alikuwa akikaa bench.
Mchezaji wa Yanga Haruna Niyonzima raia wa Rwanda hivi karibuni aliwashukuru mashabiki wa timu hiyo ,kwa kumpa sapoti kubwa wakati anpokuwa uwanjani hii inamfanya awe na nguvu wakati anapokuwa anamiliki mpirta aliuambia mtandao huu.

No comments:

Post a Comment