Tuesday, April 10, 2012

UMATI WA WATU WAJITOKEZA KWA WINGI KUAGA MWILI WA MSANII KANUMBA.

Mmoja wa wanakamati JB, akiongea na Mbunge wa John Shibuda ambaye alikuwa akimueleza kuwa kuna mwakilishi wa baba yake Marehemu kutoka Shinyaga ambaye amemwakilisha hivyo anaomba kutoa salaam.
Huu ni umati wa watu waliofurika katika kuuaga mwili wa marehemu Steven Kanumba katika Viwanja vya Leaders ,umati huu sasa unakuwa wa pili kwa wingi ukiachia ule uliofurika katika msiba wa baba wa Taifa Julius Kambalage Nyerere.
Umati huu wa watu umesababisha watu washindwe kuuaga mwili wa marehemu Steven Kanumba kutokana na msukuamano uliokuwepo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akimfariji mama wa Marehemu Steven Kanumba wakati wa Kuuaga mwili wa msanii huyo katika Ibada maalum iliyofanyika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam, hata kutokana na wingi wa watu zoezi la kuanga mwili wa marehemu limeshindikana.

Mmoja wa akina mama akiwa amezimia kutokana na kukosa hewa .

No comments:

Post a Comment