Thursday, May 24, 2012

KAMPUNI YA BIA TANZANIA KUPITIA KINYWAJI CHAKE CHA KILIMANJARO YAZINDUA KAPENI YA SHEREHEKEA KILICHO CHETU. (100 TZ FLAVE)

 Nembo  ya 100 TZ flava ambayo imezinduliwa leo kwa waandishi wa habari za michezo jijini Dar es Salaam ambayo ujumbe wake ni kusherehekea kilicho chetu.
 Baadhi ya waandishi wa Habari za michezo wakiwa wamesimama kwa muda kwa ajiri ya kumkumbuka mwandishi mwenzao wa Gazeti la Dimba, Recho aliyefariki hivi karibuni ,katika semina ya uzinduzi wa kampeni ya bia ya kilimanjaro
 Mpiga picha wa Blogs ya Sufiani mafoto Muhidin Sufian akiwa kazini wakati wa senina ya 100 Tanzania Flava, iliyoandaliwa na kampuni ya bia Tanzania kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kusherehekea kilicho chetu .Kampeni hiyo itadumu kwa zaidi ya miezi sita.
 Mkurugenzi wa Habari wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Mike Mpunza akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa 100 Tanzania Flava iliyofanyaika jijini Dar es Salaam.

 Meneja wa Bia ya Kilimanjaro,George Kavishe, akizungumza na Waandishi wa Habari za Michezo  wakati wa semina maalum kuhusu uanzishwaji, matumizi ya picha za matangazo katika uzinduzi wa Kampeni mpya ya Bia ya Kilimanjaro, inayokwenda kwa jina la 100% Tanzania Flava, iliyoandaliwa na kampuni hiyo  iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya New Afrika, Jijini Dar es Salaam. Kabla ya semina hiyo na waandishi wa habari ilianza Semina maalum kwa Wahariri wa habari za michezo kutoka Vyombo vya habari mbalimbali, Picha zao endelea chini.
 Mtangazaji wa TBC1 Angela Msangi akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
 Mkurugenzi wa Executive Solution Agrey Marealle kulia akiwa na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro George Kavishe kushoto na Mshauri wa Executive Solution Cecilia Assey katikati wakiwasiliza kwa makini maswali yaliyokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari wakati wa sherehe za uzinduzi wa 100 Tanzania Flave.
 Mkurugenzi wa Executive solution Agrey Marealle, akizungumza na Waandishi wa Habari za Michezo  wakati wa semina maalum kuhusu uanzishwaji, matumizi ya picha za matangazo katika uzinduzi wa Kampeni mpya ya Bia ya Kilimanjaro, inayokwenda kwa jina la 100% Tanzania Flava, iliyoandaliwa na kampuni hiyo  iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya New Afrika, Jijini Dar es Salaam. Kabla ya semina hiyo na waandishi wa habari ilianza Semina maalum kwa Wahariri wa habari za michezo kutoka Vyombo vya habari mbalimbali, Picha zao endelea chini.
 Wanablogger  hapa nchini wakiwa katika  semina hiyo, (kulia) ni Othman Michuzi na Bashir Nkoromo, John Badi ,wakisikiliza kwa makini hutuba ya Meneja wa Bia ya Kilimanjaro George Kavishe.
 Meneja wa Matukio wa Executive Solution Sasha Nella akiwa na Muhidini Sufiani wakati wa uzinduzi wa kampeni ya 100 Tanzznia Flava( TUSHEREHEKE KILICHO CHETU)
Wanablogger  hapa nchini wakiwa katika  semina hiyo, (kulia) ni Othman Michuzi na Bashir Nkoromo, wakiendelea na kazi ya kurusha moja ya matukio yaliyojili katika uzinduzi huo wa 100 Tanzania Flava.

No comments:

Post a Comment