Tuesday, June 5, 2012

TUNASUBILI KUONA UWEZO WA WAKUU WA WILAYA .


HIVI  karibuni Rais wa  Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete alifanya  mabadiliko  ya  uteuzi wa wakuu wa wilaya  wapya nchini  kwa lengo la kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo.

Tunaipongeza Serikali kwa kufanya hilo  kutokana na baadhi ya wakuu wa wilaya walikuwa wapo nyuma katika kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo na kuachia madaraka kwa viongozi wengine waweze kusimamia.

Hali hiyo ilikuwa ikifanya inaleta maswali mengi hivi mkuu wa wilaya anashughuli gani  katrika wilaya husika ikiwa kazi zake zinafanywa na mtu mwingine wakati huo huo mshahara anapokea kama kawaida?

Pengeni wakati wa mchujo huo nadhani suala hilo limekuwa likiangaliwa kwa umakini kutokana na wananchi wengi wamekuwa wakitoa malalamiko hawana imani na viongozi wao mabo ni wakuu wa wilaya.

Naamini  kwa baadhi ya   wilaya   ambazo wananchi walikuwa wakitoa  malalamiko ya watendaji wao ambao ni wakuu wa wilaya  na kuondolewa kabisa katika madaraka wamefurahi na kwa upande mwingine bado wana dukuduku kwa kurejeshwa kwa mkuu wa wilaya  wa zamani.

Nimekuwa shuhudu kwa kupitia vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikiripoti taarifa nyingi kuhusu wanannchi kuwakataa wakuu wao wa wilaya ambao awali walikuwa wakiongoza na kurejeshwa  kwa mara nyingine  waweze kulisukuma gurudumi hilo.

Tukiachana na hilo hali hiyo  imekuwa ikitokea katika maeneo mabalimbali  kuwepo na watendaji wabuvu katika kuhakikisha wanasimamia maendeleo ya miradi ya wanannchi wake katika wilaya husika.

Pia jukumu lingine ni pamoja na kuhakikisha kuwa maeneo yao yanakuwa na miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa viwango stahiki na nidhamu katika ukusanyaji wa mapato na matumizi ya fedha za umma na kujiridhisha kuwa zinatumika kwa manufaa ya wananchi.

Kadhalika jukukumu lingine ni pamoja na  kuhakikisha wanasimamia vizuri ukusanyaji wa mapato kwenye halmashauri zao kwa sababu ndiko viliko vyanzo vikuu vya mapato.

Katika bajeti iliyopita, halmashauri zilipanga kukusanya Sh320 bilioni lakini, hadi kufikia Januari mwaka huu, ni Sh90 bilioni tu ambazo zilikuwa zimekusanywa, na hali hiyo imetokana na kuwepo kwa usimamizi mbovu kwa baadhi ya watendaji katika  Halmashauri hizo.

Aidha  jukumu lingine ni kuhakikisha kuwa mikoa na wilaya zao zina akiba ya chakula cha kutosha na kuwa  na fursa za kuzalisha mazao mbadala , na   kumizeni watu wao walime mazao yanayostahimili ukame, yanayokomaa kwa muda mfupi na hata kuwasisitiza wazalishe chakula cha ziada ili wawe na akiba ya kutosha na pia waweze kuuza na kupata fedha.

Kilichonifanya  kuandika suala hili  pamoja na  wananchi wa wilaya ya Iramba wamekuwa wakitoa malalamiko yao inakuwaje   mwanafunzi  wa chuo Kikuu Finland  ambaye anatarajia  kumaliza masomo yake mwaka 2014. ambaye kachaguliwa kuwa mkuu wa  wilaya.

Kutokana na hivi sasa yupo  masomoni  na bado ana miaka miwili ya kumaliza je kwa muda huo nani atakuwa anafanya  yale majukumu yake na mshahara atalipwa  wakati yupo huko?  Na hata hivyo   sasa hapa kuna maswali  mengi  yanakuja  watajigawa vipi katika kusimamia  miradi ya maendeleo  ya wananchi?

Hata nilipata fursa ya kusikiliza majibu ya mkuu huyo  katika mahojiano ya Televisheni ya TBC1 alisema kuwa ataweza kuugawa  muda wake  ili kuhakikisha wananchi wanapata waki zao za msingi na yeye anajipatia haki yake ya  kupata elimu.

La asha kulingana na  majibu yake sikuweza kupata jibu la haraharaka  na kuanza kujiuliza muda gani atakaoutenga kwa ajili ya kusimamia  miradi ya maendeleo   na kuwatumikia  wananchi wake akiwa huku nje.

No comments:

Post a Comment